BUSOKA NA KUCHELEWA
Na .OBERT FUNGA.
KAHAMA.
1/03/2015..
ELIMU
Wakazi wa kata ya busoka iliopo katika halmashauri ya mji
wa kahama wilayani hapa,wameulalamikia uongozi wa wilaya hiyo kwa kushindwa kuifungua shule ya secondari
ya wasichana kata ya busoka ‘’baba haji busoka’’.
Wakazi hao walisema licha ya kukamilisha ujenzi uliojengwa na kampuni ya NIDA Textile Mills ambayo ilianza mchakato
huo 2008/2009 na kukamilisha ujenzi wa shule hiyo 2010 ambayo ni kwa ajiri ya wasichana kuanzia kidato cha kwanza hadi cha
sita.
Mwaka 2011 kampuni ya NIDA ilikabidhi shule hiyo katika
uongozi wa halmashauri ya mji wa kahama
zaidi ya miaka 6 iliopita mpaka
sasa haijafunguliwa bila sababu za
msingi na imeshindwa kuifungua shule hiyo.
Kaimu meneja wa NIDA- Edson peter alisema serikali na halmashauri ya mji wa kahama kuna
jambo la sintofahamu kwa kushindwa kuendeleza
shule hiyo tulioikamilisha ujenzi uliogharimu kiasi cha Tshs,250 milion
[CASH MONEY]
Peter aliongeza tumejitoa kimasomaso kukamilisha vyumba
vya madarasa 15 yenye kila kitu kwa jinsi
ilivyokusudiwa tangu 2011 tulipoikabidhi halmashauri ya mji imeshindwa
kuiendeleza na sasa imetelekezwa.
‘’’Kuna mambo ya siasa ambayo yanaingizwa kwenye elimu kutoka kwa mkuu wa
wilaya ya kahama benson mpesya ,,mbunge
wa jimbo la kahama james lembeli na
wakuu wa idara ya elimu,waratibu
elimu kanda ya ziwa,ofisa elimu wilaya
hii’’’alisema kwa masikitiko Peter
Baada ya kujenga shule hiyo mwekezaji aliomba iitwe jina la baba haji busoka,kama kumbukumbu ya
mtoaji wa misaada yenye tija katika wilaya ya kahama na nchini kwa ujumla.
Mkuu wa wilaya ya kahama benson mpesya alisema
kutofunguliwa kwa wakati kwa shule hiyo
kuna sababu 2, mgodi wa bulyanhulu[acacia] kitengo cha miradi kimeyumba kutoa
mahitaji muhimu,makubaliano baina ya
serikali ya wilaya na mwekezaji
yaliyumba kimpangokazi.
Mpesya alisema mgodi wa bulyanhulu[acacia] uliingia makubaliano ya ujenzi wa nyumba za walimu ili shule hiyo iweze
kufunguliwa baada ya NIDA Tixtile Mills kujitolea madarasa 15.
Makubaliano ya mgodi yalikuwa ni kusaidia vifaa vyote vya
ujenzi na halmashauri ya mji wa kahama
itafute mkandarasi wa ujenzi ambapo wote 2 hawajakamilisha kusudio kamili.
Mpesya aliongeza ya kuwa meneja miradi wa mgodi wa
bulyanhulu Giten Givecha ameshinwa kuonyesha ushirikiano kwa kukamilisha ujenzi
wa nyumba za walimu na vifaa vingine.
Kwa upande wa mkurungenzi mtendaji wa halmashauri ya mji
wa kahama Felix kimaryo alisema itafunguliwa
iwapo ofisi ya elimu kanda ya ziwa kufanya ukaguuzi na mambo yote yatakuwa
kamilifu shule hiyo itaanza kutumika ‘’’
miaka sita haijakamilika……NI lini
Itakamilika??????’’’.
…………..MWISHO…………..
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni