WATOTO MITAANI NA VIJANA WAJASILIAMALI
Obert funga.
Kahama.
01/03/2015.
WATOTO
Halmashauri ya mji wa kahama
wilayani hapa,imetakiwa kuwakumbuka watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi
na mazingira magumu waliopo katika standi za basi,majumba yasio kamilika
warudishwe makwao.
Wito huo ulitolewa jana katika
sherehe ya tathimini ya 2014 na katibu wa umoja wa wazee kahama UWAKA paul
nkwabi alisema watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi kipindi hiki cha
masika ni kibaya kwa magojwa.
Nkwabi alisema watoto
wanaoishi katika mazingira hatarishi ni zaidi ya 106 kwa takwimu za taasisi za
utetezi wa haki za binadamu SHIHABI,TALEIN na care Intenational pia hata kituo
cha mvumwa kilichopo kata ya nyahanga.
‘’serikali isitafute lawama
kwa UWAKA wakati haifanyi wajibu unaostahiki mpaka tuwe tunawaambia kila jambo
watoto hao wanalala kwenye vibaraza vya maduka,kwenye majumba mabovu,kwenye
mitalo na sehemu za hatari.
Kwa upande wa mwenyekiti wa
CCM mkoa wa shinyanga Khamisi mgeja ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe
hiyo alisema naunga mkono kwa 100% jambo hili lifanyiwe uharaka kwa kuwarudisha
makwao watoto hao.
Wanahangaika watoto hawa kwa
njaa,maradhi,malezi na sehemu ya kulala, serikali ifanye mchakato wa haraka
ikisaidiana na taasisi za haki za binadamu,dawati la jinsia,vituo vya kulelea
watoto na mashirika mengineyo.
Mkurugenzi mtendaji wa mji
felix kimaryo alisema jambo hili la kuwarudisha watoto linafanyika na litakuwa
endelevu mpaka mwezi wa 21/3/2015 na tutatoa takwimu halisia ya watoto waliorudishwa
na waliobaki.
…………MWISHO…………
Obert funga.
Kahama.
01/03/2015.
VIJANA
Kikundi cha ujasilimali cha
vijana na maendeleo kilichopo katika kata ya nyihogo wilayani kahama mkoani
shinyanga,wamepewa mchango wa kuku 500 na wakili nkuba kwa kukijenga na
kukiendeleza kikundi hicho kwa hali ya upendo.
Hali hiyo ilijitokeza jana
kwenye sherehe ya kikundi cha vijana na maendeleo ambapo mgeni rasmi wa kikundi
hicho alikuwa Wakili Nkuba ambaye aliambatana na katibu wa mbunge wa jimbo la
kahama Abdul Ntahokaja.
Awali kikundi cha vijana na
maendeleo kilisoma risala kwa mgeni rasmi na wageni walikwa kwa mapungufu na
changamoto za mahitaji na malengo
makubwa ya kukamilisha kikundi ili kiwezekukidhi mradi kusudiwa.
Mwenyekiti wa kikundi cha vijana
na maendeleo Yohana Jackson aliyesoma risala alisema tumebuni mradi wa ufugaji
wa kuku licha ya kujishughulisha na ajira za photo copy,ushonaji
vitambaa,biashara ndogondogo na kukopeshana mchango.
Mgeni rasmi aliahidi kutoa
kuku 500 endapo ujenzi wa banda utakapo kamilika na kuwapa ushauri wa kujiandaa
na maandalizi ya ufugaji wa kuku kwa magonjwa,ajali,kung’atwa na
nyoka,lishe,pahala safi na huduma stahiki.
Naye katibu wa mbunge abdul
ntahokaja alisema nimetumwa na mbunge james lembeli kuwakilisha kiasi cha fedha
Tsh,1000,000 kama mchango wa kikundi cha vijana na maendeleo kilicho mwandikia barua ya kumkaribisha
ashiriki katika sherehe ya ufunguzi.
Aidha ntahokaja alisema
mbunge amekwenda arusha kwa shughuli za kitaifa lakini ameona hawezi kuacha
kufika ndiyo maana nimefika mimi badala yake pia hakijaharibika kitu,fedha za
mchango wa vijana wanaojituma,kujiajiri na kuweka ujasiliamali kwa kujiamini
zipo.
………….MWISHO……………
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni