Obert funga.
Kahama.
2/03/2015
Mjumbe wa kamati kuu taifa katika
halmashauri ya mji wa kahama wilayani kahama mkoani shinyanga Sebastiani Tobias
[komaa] amewatahadharisha wenyeviti wa mtaa wa nyihogo na mtaa wa sazia ya kuwa
wawe makini kwa fitina za ccm.
Akiwahutubia wananchi katika hafla
iliofanyikika katika viwanja vya nyihogo soko la miwa bw, sebastiani alisema
tumefanya hafla ya kuwashukru wenyeviti wa mitaa kutokana na mateso ya ccm tukiwa katika hali mbaya ya
wizi,dhuluma,manyanyaso na kubezwa.
‘’bado miezi michache ya kuingia
kwenye harakati za uchaguzi fitina za ccm kuwe na umakini wa kufanya harakati za maendeleo na vita ya vyama
bila ya kuwa na jitihada za ziada kutakuwa na mchezo mchafu’’alisema.
Sebastini aliongeza Chadema
imejipanga vyema katika uchaguzi mkuu wa mwezi 10 kwa matokeo ya kufurahika,
tutaanza kutazama daftari la wapiga kula,vitambulisho vya
kupigia kula na maandalizi yatakayo
tulidhisha bila hivyo kitaeleweka mpaka chadema iwe na uhuru.
Aidha mwenyekiti wa chadema
wilaya ya kahama juma protas ntahipera alisema mwezi wa 2 watampeleka mahakamani aliyekuwa mwenyekiti wa mtaa wa majengo
bw,mseveni mukula kwa dhuluma ya fedha za michango na kujichukulia maeneo ya
ardhi.
Hata hivyo hafla hiyo
ilivulugika mara baada ya kuja vijana wa mitaani kwa kunyang’anya chakula kwa
akinamama wapishi ikiwemo kamati ya maandalizi kushindwa kuithibiti vulugu ya
vijana hao licha ya kuwa na brigedi 10 [askari] wa chama cha chadema.
Mpaka muda wa 12:48 jioni
chakula kilichopikwa ni sufuria 7 za chakula
sufuria 3 za nyama, kilikuwa kimeliwa na vijana zaidi ya 140 na kubakiwa na
sufuria 1 la wali ambalo wapishi walisusa kula walitaka walipwe pesa ya upishi.
……………Mwisho…………..
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni