Jumatatu, 2 Machi 2015

NGUMI 1



Na .Obert  funga.

 Kahama.

2/03/2015.                     VURUGU  CCM

Wakati homa ya uchanguzi mkuu wa rais,wabunge,madiwani ikiwa inaanza kupanda,viongozi wa [CCM] na umoja wa wzee kahama UWAKA kata ya malunga wilaya ya kahama mkoani shinyanga wameanza mgogoro wa  kutuhumiana.

Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa CCM kata ya malunga Donard Iguru alisema chanzo cha kunyosheana vidole na umoja wa wazee kata ya malunga [UWAKA-Kata] na kukaa vikao viwili vya usululishi ambapo bado maneno yanatokea ya uongozi wa kata kuto waheshimu wazee.

Awali kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa wazee wa [uwaka] john ngassa na  phil lugwalalira waliingilia  madaraka ya uongozi wa CCM kata ya malunga kwa kuwachagulia wenyeviti waliokuwa wakigombea  mitaa wanaotoka [chadema] bila kuiweka ccm katika orodha nzuri.

Iguru aliongeza ya kuwa John ngassa yeye ni chadema anatuchagulia vijana wake wa chadema na kutulazimisha tuwasimamishe kugombea uongozi wakati ccm tunajiweza anatuambia yeye kama mzee wa UWAKA anamaamuzi ya kutuambia jambo la chama bia kufuata sheria na sera za chama .

CCM iliwachagua vijana wanaofaa kwa uongozi wa serikali ya mtaa lakini tumeshinda mtaa wa korogwe mwenyeviti Edward makomba kati mitaa 3 ya Igomelo na malunga ambayo tumenyang’anywa na chama cha upinzani.

 Baada ya matokeo ya uchaguzi yalioanza 14/12/2014 kulitokea kutoelewana‘’tulifanya kikao cha kuombeana msamaha’’Tuliwaarika mwenyekiti wa UWAKA wa wilaya ya kahama Mashaka kilonda pia upande wa CCM Tulimuomba aje katibu mwenezi wilaya bw, Masud Merimeri lakini wazee walimkataa masud merimeri.

Wazee hao walifanya kikao na watu hao binafsi cha kumzodoa mwenyekiti wa mtaa korogwe Edward makomba CCM wakahamia kwa katibu mwenezi wilaya   masud merimeri ya kuwa ni mla rushwa wa tozo za ushuru wa Jengo la CCM wilaya.

 Hata hivyo wazee hao ambao hawajui kanuni na sheria zilizopo katika katiba ya UWAKA,pia CCM kwa fedha za wapangaji wa vyumba wazee hao walisema TAKUKURU hawakumchunguza vyema masud merimeri 2013/2014 wakati sakata lilikuwa la kumtia hatiani.alisema Iguru

Mwenyekiti wa umoja wa wzee kahama[UWAKA]- Mashaka kilonda alisema viongozi wa CCM malunga kusigana na wazee wa uwaka ni uroho wa madaraka na tamaa isiokuwa na ubusara kwa kufanyiana umangimeza usio na tija ya kisiasa.

                             ………..MWISHO………

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni