Obert funga.
Kahama.
28/02/2015.
FEDHA ZA UCHAGUZI
Mwenyekiti wa mtaa wa igalilimi kata ya kahama mjini
wilayani hapa mkoani shinyanga, Bw,Ibrahimu Can Wally [CCM] ameshitakiwa
mahakama ya mwanzo kwa kudaiwa fedha alizokopeshwa 12/06/2014 zilizodaiwa ni
kwa ajiri ya kufanyia kapeni ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika 2014.
Mfanyabiashara Bw,Sikujua
Ndoi alimshitaki katika mahakama ya mwanzo kwa madai ya kumkopesha fedha zaidi
ya Tshs milioni 4.5 kwa kufanya kampeni ya uchaguzi wa serikali za mitaa
uliomalizika 14/12/2014 na matokeo yakatoka akawa mshindi katika mtaa wa
Igalilimi.
Awali mfanyabiashara
Bw,Sikujua Ndoi alisema nimekuwa mpangaji wa chumba hiki zaidi ya miaka 10 kwa
Bw,Ibrahim Cann amekuwa kama ndugu pia nimekuwa nikimwamini kwa ushirikiano wa
kuheshimiana, Sasa alikuja hapa kunikopa
fedha ile heshima sikumnyima.
Nakumbuka 01/2/2013 alianza kuniambia kuhusiana na
kumkopa fedha za kupigia kampeni za uchaguzi wa serikali za mtaa ilibidi
tutafute watu wa heshima ili nimkabidhi kwa ushahidi wa kutosha,kweli jambo
likafanyika kama tulivyoambizana tukapeana mbele ya watu 5.
‘’’Barua kumb no,brz/10/3/02
iliotoka baraza la kata ya kahama mjini kwenda kwa mfanyabiashara Sikujua Ndoi kwa
kunishitaki nitoke kwenye chumba 28/2/2015
bila sababu za msingi,barua hii ilinifanya nikimbilie mahakamani na kumfungulia
kesi ya madai ya fedha zangu anilipe’’’alisema.
Kwa upande wa mwenyekiti wa
mtaa ambaye pia ni mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wilaya [CCM] Bw,Ibrahimu
wally canny alivyohojiwa na waandishi wa habari kuhusiana na kukopa fedha kwa
mfanyabiashara alisema mimi nachojua ni mpangaji wangu kama mambo ya mahakamani
siwezi nikayasema jinsi yatakavyokuwa na
habari ya fedha kumkopa itajulikana mahakamani sina kauli zaidi ya hiyo.
………………MWISHO………………
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni