LEMBELI NA NGUO
Obert funga.
Kahama.
2/03/2015. SOSOPI asema Bavicha
Chama cha demokrasia na
maendeleo ‘Chadema’wilayani kahama mkoani Shinyanga,kimemtaka mbunge wa jimbo la kahama Bw,James Lembeli
ajiweke kwenye msimamo wa kujionyesha kutokana
na maamuzi yake ya kukataa kila jambo linalotokea ndani ya ccm.
Akizungumza katika mkutano
uliofanyika kata ya nyihogo katika viwanja vya Bwawani makamu mwenyekiti wa
[Bavicha]Bw,Patrick Ole Sosopi alisema harakati za Samweli Sitta,James Lembeli
na harrson mwakyembe ilikuwa na ajenda kwa watanzania lakini imezimwa kwa
kufanyiana hujuma ilioanza kwa mwakyembe.
Bw,Sosopi aliongeza ya kuwa
Lembeli amekuwa ccm kwa bahati mbaya toka awali alikuwa na majibu ya kuwa
tofauti na malengo ya ccm ndiyo maana hakuna Utekelezaji wa kauli ya Rais
aliosema akaikubali.
Kamati ya maadili ya ccm
ilimtishia kumnyang’anya kadi alijibu ‘’ccm sio mama yangu’’sakata la Uwaziri
wa maige alipiga msumari mkali,tokomeza ujagili wana ccm kawamwaga,katiba ya
jaji walioba,escrow na kuwekwa kiporo kwa peter mhongo vyote kamkana Rais
kaikana ccm.
‘’’imekuwa kawaida kwa
mbunge wa jimbo la kahama na mbunge wa jimbo la msalala kuungana na hoja za
chadema zikitolewa bungeni zaidi ya miaka yote waliokuwa wana ungamkono kwa
100%’’’alisema
Aidha Bw,Sosopi alisisitiza
kwa kuwaambia wananchi ya kuwa viongozi wote waliokwenda loliondo kwa babu
Ambilikile mwasapile kunywa dawa ndiyo wenye kuto tekeleza wajibu wa maendeleo
kama mbunge Lembeli ambaye jimbo la kahama hakuna kumbukumbu zaidi ya saccos 3.
Licha ya kutumia mfuko wa jimbo kwa miradi
mbalimbali kwa kuchangia shule,kikundi,zahanati,nyumba za walimu na ofisi
mbalimbali lakini hakuna majibu ya Uhakika ya matekelezo kutokana na eneo
husika kuwa vilevile kama alivyolikuta na hakuna afisa mtendaji aliye mshitaki.
Tunataka Lembeli afanye
mrejesho wa kila pahala alipotoa mchango wa mfuko wa jimbo atoe majibu kama
halmashauri ya ushetu kuna kata 6 zimechukua michango lakini hakuna matekelezo
pia halmashauri ya mji kuna kata 7 hakuna utekelezaji.
………………..MWISHO………………….
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni