mwalimu wa shule ya msingi kinamapula
Obert funga.
Kahama.
2/03/2015.
MWALIMU AKIMBIA TUKIO
Mwalimu wa shule ya msingi
kinamapula Burugu Kayagira[wakujitolea] iliopo kata ya kinamapula katika
halmashauri ya ushetu wilayani kahama mkoani shinyanga,amekimbia katika eneo la
kazi mara baada ya kuwadhibu wanafunzi wa darasa la saba.
Wanafunzi waliojeruhiwa
vidoleni ni 3 na waliojeluhiwa maeneo mbalimbali ni 3 kwa kukaidi amri ya
mwalimu huyo ya kuwalazimisha kuzoa kinyesi kwa mikono wanafunzi hao
wakishirikiana na mwalimu wa zamu zuhura mboja.
Hata hivyo wazazi
wakilieleza gazeti hili ya kuwa wanafunzi waliopigwa viboko zaidi ni wanafunzi 6 kuliko wengine
ambao walikubali kushika kwa mikono bila kutumia kifaa cha aina yeyote.
Awali 19,02,2015 muda wa
asubuhi katika shule hiyo kulitokea tukio la kuona vinyesi vingi vya watu
wakubwa katika darasa la saba ambavyo vilionekana ni ushirikina uliopo katika
shule hiyo.
Mwalimu Burugu Kayagira
aliwaadhibu wanafunzi hao kwa kutotii amri yake aliowaelekeza ya kuzoa kwa
mikono vinyesi hivyo ndipo alianza adhabu ya kuwapiga kwa mfululizo wa viboko
maeneo mbalimbali na kusababisha wanafunzi 3 kuumia vibaya na wengine 3 kuumia
mikononi.
Mwenyekiti wa shule ya
msingi ya kinamapula Bw,Elias Kachembe aliliambia gazeti hili ya kuwa turifanya
kikao cha dharula kwa ajiri ya mgogoro huu lakini wazazi walikuwa na dhamira ya
kumshitaki huyu mwalimu ndipo alikimbia mpaka sasa hatujui alipokimbilia.
’’’jambo la kuwalazimisha halikuwepo isipokuwa adhabu ya viboko ndiyo
iliomgharimu kwa kuwapiga kiasi cha kuumia lakini nao wazazi wanakuja mbiombio
kufanya ugomvi bila busara ya kumwita mwalimu mkuu au mimi tukae kwa kujadili
kilicho tokea’’’alisema.
Mwalimu mkuu Vumilia Ndessi
alitafutwa kwa njia ya simu-kujibu yaliotokea shuleni kwake alikiri ya kuwa
kweli kulitokea adhabu ya namna hiyo lakini mwalimu burugu kayagira aliyekuwa
kwenye kipindi cha asubuhi darasa la saba amekimbia bado ajaripoti ofisini.
Kaimu afisa elimu msingi
wilayani hapa Bw,Silvanus Bonda alisema ni mara ya pili shule hii kuletewa
malalamiko ya kuhusiana na walimu,wanafunzi kuteswa,kamati ya shule kutofuata
utaratibu uliopagwa na mihtasari ya
ajenda kuikamilisha kama lengo la mikakati.
‘’’jambo hili litakuwa
limenizidi uwezo wangu mpaka viongozi wa juu maana hao ndiyo litakamilika kwa
kuona wapi pana ulegevu kutoka ya 2014 na ya sasa 2015 kufuatana na mihtasari
ya vikao na taarifa iliofika kwenye ofisi ya mkurugenzi’’’alisema.
Aidha kaimu afisa elimu
alisema kuna jambo lenye utata kwa mikakati ya juhudi ya kulimaliza ‘gogoro’ la
aina hii bado kuliweka sawa kwa vile hatujakutana tulijue mwanzo na mpaka
kufika lilipo tutalifanyia kazi baada ya kukaa kikao cha pamoja.
…………MWISHO………….
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni