Jumanne, 31 Machi 2015

WAGANGA WANAO ANDAMWA NA WANANCHI



Obert  funga.

Kahama.

31/03/2015.                      Waganga  wa kienyeji

Wakazi wa kijiji cha mwakata na Igugunwa  katika kata ya Isaka wilayani hapa mkoani shinyanga wamewalalamikia jeshi la polisi kwa azma ya kuwakamata waganga wa kienyeji wapiga ramli chonganishi huku wakiachwa waganga wa kienyeji 2 bila sababu yeyote.

licha ya serikali na wahisani mbalimbali kutoa misaada ya pesa,vifaa,vyombo na ujenzi wa nyumba za haraka kwa waadhirika wa majanga ya mvua ya mawe ilioikumba kijiji cha mwakata na Igugunwa kuua wananchi 48 na majeruhi 118 huku ikiwaacha wakazi 512 wakiwa hawana pa kuishi mpaka sasa utaratibu unafanyika wa kuwajengea eneo lenye maakazi.

Makizungumza kwa nyakati tofauti katika kijiji hicho walisema tupo katika kuweka jambo hili kwenye tahadhari ya waganga wa kienyeji waliosalia kwa mtafaluko uliokuwepo mwanzo kwa madai ya michango ya dua ya mvua iliochangishwa na waganga 2 kati ya kamati ya wazee 19 alisema Sofia Shija mkazi wa mwakata.

Awali kulikuwa na michango ya kamati ya wazee waomba dua ya mvua tokea 23/01/2015 ambayo kamati ina wazee 19 iliotufanya tuchange michango mbalimbali zaidi ya mara 3 kwa wachangishaji waliotuletea tangazo la kikao cha dua ya mvua.alisema Bi,Sofia

Naye Shabani ng’anghu mkazi wa kijiji hicho alisema hasira ya mganga wa kienyeji [mwanamaria]aliyeuawa na wanakijiji kwa kutoongea ukweli wa jambo la kuchangisha michango ya mvua mpaka maamuzi magumu ya wanakijiji kumvamia mganga huyo na kuumua.

‘’’sasa kuna nini jeshi la polisi kutowakamata waganga wa kienyeji wapiga ramli chonganishi Machimu Mwanandalo na Zingu Mwanazingula wakati hawa wapo katika kamati ya wazee waomba dua ya mvua pia ndiyo waliotuambia wananchi tuchange michango ya pesa,nafaka,nguo nyeusi au nyeupe kwa ajiri ya uombaji wa dua ya mvua’’’alisema ng’anghu

Hata hivyo wanakijiji hao walipaza sauti kwa ujumula ya kuwa wanahitaji kukamatwa kwa waganga hao ili kuwe na Imani na maafa yaliotokea 03/03/2015 saa 3:30 usiku kuwa ya mungu mwenyewe na  sio ya  kishirikina kama inavyosemekana kutokana  na mgogoro uliokuwepo mwanzo wa waganga wa kienyeji na wanakijiji kudai mvua walioichangisha michango.

Mwenyekiti wa kijiji cha mwakata Ezekial Saanane alivyohojiwa kuhusiana na maamuzi ya wanakijiji kuhitaji kukamatwa kwa waganga wa kienyeji wapiga ramli chonganishi alisema kwa sasa nipo katika harakati za kwenye majukumu ya kupokea wageni na watoa msaada hali hii ya wanakijiji kuchukua uamuzi huo ni kwa ajiri ya kupata jumuiko la kuweka  usahihi wa tukio la hivi karibuni.

‘’’Mvua ya mawe ilionyesha katika kijiji cha mwakata 03/03/2015 Saa 3:30 Usiku imereta Imani tofauti kati ya waganga na wazee wa kijiji hicho kufanya TAMBIKO la kuomba mvua ya kawaida waliokuwa wanaitaka inyeshe katika kijiji cha mwakata  na vijiji vingine na imekuja mvua isio na matarajio ya  kufanya uharibifu mkubwa wa mali,mazao,mifugo na nyumba kuharibika tuwe  wazi katika kuisemea serikali’’’alisema mwenyekiti.

Kamanda wa mkoa wa Shinyanga Justen Kamugisha alivyohojiwa na waandishi wa habari kuhusiana na kuwakamata waganga wa kienyeji wapiga ramli chonganishi 2 alisema jambo hili la waganga wa jadi wapiga ramli chonganishi ni la utaratibu wa tulioupanga na kutolea maamuzi ya kisheria kutokana na mambo ya mauaji ya vikongwe,albino,mauaji ya kuchukua viungo vya binadamu.

Jambo la waganga wa kienyeji wa mwakata ambao wanakijiji wanataka tuwakamate na kuwafikisha katika vyombo vya sheria tunaomba watulie na waje katika ofisi zetu ilikupata uhakika wa Mwanandalo na Mwanazingula wanaotakiwa tuwakamate kwa utaratibu wa aina ipi wakati polisi ina utaratibu na maamuzi yake.

Aidha kamanda Kamugisha alisisitiza ya kuwa kuna utaratibu waganga wa kienyeji wanatakiwa waufuate na si vingine kamata kamata ya waganga wa kienyeji Inaendelea katika kata zote za mkoa wa Shinyanga ambapo tutatoa orodha ya yote ya waganga wa kienyeji wenye nyara za serikali,viungo vya binadamu na mauaji ya albino tutawapeleka mahakamani.

         ……………………..MWISHO…………………..

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni