Jumatatu, 2 Machi 2015

UKUNE HOI



Na.obert  funga.

Kahama.

2/03/2015.                                                         UKUNE BILA HUDUMA

Waakazi wa kata ya ukune iliopo katika halmashauri  ya ushetu wilayani kahama mkoani shinyanga,wameitaka taasisi ya mkapa foundation kusitisha shughuli zao katika kata hiyo kutokana na kuutoona faida ya taasisi hiyo iliofanyika mwaka 2014.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika kata hiyo Bi,Zuhura  James alisema taasisi ya mkapa foundation ilikuja ukune pamoja na idara ya afya kwa ajiri ya harambee ya uzinduzi wa vyumba vya upasuaji na damu salama katika kituo cha afya chenye kusuasua.

 Taasisi hiyo inayojishughulisha na masuala ya afya tumekuwa tukisumbuka kwa hali ya malipo ya afya tulijua harambee iliokuwepo itatusaidia wana ukune kumbe iliofanya harambee ya Tshs milioni 5 zilizochangwa mwaka 2013/2014 ilikuwa change la macho.alisema

Naye bw,Hamisi Kujakumbhi alisema matumizi ya fedha zile za harambee pamoja na fedha za mfuko wa jimbo na mchango wa mbunge wa jimbo bw,James lembeli alitutangazia mchango wake kwa kata ya ukune yalitakiwa tutambue wananchi wa ukune yapo wapi.?

‘’’kaimu mganga mkuu wa wilaya ya kahama bw,Dr john nduttu alisema harambee ya ukune iligharimu   mipango kazi kwa Tshs milioni 507 ikiwa na mikakati ya idara ya afya,wizara na taasisi ya mkapa foundation ili ifikapo mwezi juni 2015 tuwe tumekamilisha.

 Hata hivyo Dr nduttu alisema Kituo cha afya cha ukune kweli harambee ilifanyika ya kuchangia vyumba vya upasuaji ambapo taasisi ya mkapa foundation,mfuko wa jimbo,wananchi walisaidia kuiweka pahala pa kuweza kupata huduma ya afya ilio bora’’’’alisema Dr,nduttu

Diwani wa kata ya Ukune sayi  gamaya alisema natambua uongozi wa halmashauri ya ushetu akiwemo kaimu mganga mkuu na mbunge wa jimbo la kahama kwa harambee ile kata yangu haijatendewa haki wakati taasisi ya mkapa foundation ilifika kwa uondoa usumbufu.

‘’’Kata ya ukune wananchi wanaona diwani ndiyo kala fedha zilizochangwa,wauguzi na manesi nao kama wa kukopwa kaimu mganga mkuu anadai fedha zilikuwa kidogo mipango haikufanyika kwa wakati ila kwa sasa tusubiri utaratibu na matunda ya michango’’’’,

Aidha diwani Gamaya aliongeza ya kuwa taasisi hiyo ilitoa maelezo ya kuwa fedha hizo zilizizochangwa na halmashauri kunakurejeshwa kwa matumizi ya kuboresha huduma ya afya lakini imekuwa siasa ya uongozi wa halmashauri na taasisi hiyo.

Mkurugenzi wa halmashauri ya ushetu Bi,Isabela chilumba alivyoulizwa kuhusiana na suala la harambee ya kata ya Ukune kwa kudorola katika kituo cha afya cha Ukune alisema siyajui ya ukune maana sikuwepo katika harambee hiyo.

                      ………………..MWISHO………………

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni