Jumamosi, 18 Aprili 2015

AJALI ZAWA KAMA JANA NA LEO

KITENDO    CHA   MFULULIZO   WA  AJALI   HAKUNA   KIONGOZI    ALIYE   KUNA   KICHWA      KWA  KUNUSURU    WAPO   WATOA   POLE....................   HIII   TZ


Habari kutoka mkoani Mbeya zinasema kuwa watu zaidi ya 18 wamefariki dunia papo hapo baada ya Hiace waliyokuwa wanasafiri nayo kupata ajali katika  eneo la uwanja wa ndege Kiwira wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya.
Inadaiwa kuwa gari hiyo imetumbukia katika mto wa Kiwira,wilayani Rungwe mkoani Mbeya.
 
Hiace ikiwa mtoni


Hiace ikiwa mtoni
Mpaka sasa Miili ya watu 22 imefanikiwa kutolewa kwani Hiace ilitumbukia mtoni ambapo miili mingine imenaswa na juhudi za kuitoa inafanyika.Katika jali hiyo inasemekana watu wawili tu ndiyo wamepona akiwemo kondakta.


Taarifa zaidi tutawaletea hivi punde

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni