Obert
funga.
Kahama.
5/4/2015. Wajibu wa
polisi
Jeshi la
polisi wilayani kahama mkoani hapa linadaiwa kabiliana na changamoto za
utendaji hafifu katika wajibu wa kipolisi na kuwa na wakuu wa polisi
wilaya’OCD’wakuu wa vituo’OCS’ wasiofuata matendo ya kazi yao na kuchangia kiwango
kikubwa cha kuhamishwa.
Hayo
yalisemwa jana na umoja wa wazee wilaya ya kahama UWAKA ofisini hapo wakati wa
tathimini ya mchango wa jeshi la polisi kupitia kwa OCD,OCS katika ushirikiano
wa mambo ya kijamii na kuwa pamoja kwenye vikao,mikutano,jitihada za kamati za
ulinzi na usalama.
Katibu wa
uwaka wilaya ya kahama Bw,Paul Nkwabi Ntelya alisema tumekuwa na vikao vingi
vya kuwaarika waje kwenye vikao lakini hawafiki hata kutuma mwakirishi hakuna
pia sio mara moja kuna mambo yanatokea kwetu kama uwaka yanayohusu jeshi la
polisi na wananchi wa kahama tukiwa nala kuisemea jeshi hilo linakuwa kimya
bila kufika eneo husika.
‘’Tunamshukuru
IGP Mangu kwa kumhamisha ‘OCS’ Osante
Ullomi kwa mambo aliokuwa kafanya hayaendani na wajibu wa ukuu wa Idara
aliopewa,tangu hamisha hamisha ya OCD/OCS aliyeijenga kahama kwa maadili ya
kumkumbuka vyema OCD ‘P- Malengo’ tunamtazamo wa kitendaji OCD aliyebaki
Leonard nyandahu hajamfikia hata aliyekuwa [ocd]2011/14 George Simba’’alisema
ntelya.
Tumekuwa na
miariko kadhaa ya vikao vyetu tumewaarika jeshi la polisi tumeona hawafiki na
hawatumii mshirika yeyote mpaka hivi leo hakuna aliyewahi kufikakwenye vikao
vyetu hadi leo hii tuliamua kumwandikia barua ya malalamiko kamanda wa mkoa
Justus Kamugisha lakini hakuna majibu ya moja kwa moja ya utendaji mzuri wa OCS
na OCS mwenye kujitolea kama wale OCS na OCD wa 2004-2008.
Bw NtelATya
alisisitiza ya kuwa licha ya uteuzi wa wakuu wa Idara za jeshi la polisi
uendane na ushirikiano na wenyeji uliowakuta utakaofanyanao kazi na wazee wenye
ushauri wa kijumla kwa kufuata taratibu za eneo husika na kamati tendaji ya
UWAKA endapo jeshi la polisi litaarikwa kwenye vikao,mikutano na sehemu
nyingine.
Naye mjumbe
wa uwaka kata ya malunga Bw,John Ngassa alisema tunapata taarifa mbaya za jeshi
la polisi kwa mienendo ya ukiukwaji wa sheria na taratibu za jeshi la polisi
katika kituo cha polisi cha kahama kupiga kupita kiasi,kuua,kutesa,kutishia pia
kukataa kuandika maelezo ya mashitaka na kukubambika kesi.
‘’kama
unashitaka baadhi ya polisi wenye tamaa ukitaka kutoa maelezo ya kesi unaambiwa
kanunue karatasi au unashingapi nikuandikie haraka halafu unaitiwa mgambo nae
anataka pesa 20,000 kumkamata mharifu kwa utaratibu wa OCS hata ukienda kulalamika
hata kusaidia na wengi tatizo hili hajawasaidia na ndiyo maana tumefurahi
kuondoka ‘[OCS’ Osante Ullomi-alisema ngassa.
Bw,ngassa
alisema mtiririko wa uteuzi wa jeshi la polisi katika wilaya ya kahama 2008/2011ulikuwa
na imani kubwa kwa wananchi na kufanya ushirikiano wa kijamii sehemu zote sio
wakuu wa Idara ya kipolisi wa 2012/14 wenye kuandika kumbukumbu mbaya
waliobadirishwa zaidi ya 4-5 kwa kasoro mbalimbali.
………………..MWISHO…………………
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni