Alhamisi, 9 Aprili 2015

KANISA KATORIKI KAHAMA MJINI



Obert   funga.
kahama.
9/4/2015
                                           .tuhumaya Katekista
Kanisa katoriki parokia ya Mt.Kalori Lwanga jimbo la katoriki kahama katika kata ya kahama mjini wilayani hapa mkoani shinyanga, limeingia tena   kwenye  kashfa ya michango holela ilioanza 2012-2015 inayochangishwa na Kateksta Samson magoke bila uongozi  wa jimbo kulitambua.

Waumini wa kanisa katorikIi mt.karoli lwanga jimbo la kahama wakizungumza na waandishi wa habari walisema tumekuwa na mgogoro na Kateksta Magoke kwa fedha  za  michango ya wapiga picha wanazotozwa waingiapo kanisani kupiga picha  za matukio ya Sakramenti,Ubatizo,Misa  mbalimbali hatoi  jibu la kueleweka  kwa  kuwaeleza  waumini zinafanya  kazi gani?  Zipo  kigango  kipi? Au benki   ipi? Zimefikia  kiasi  gani ? pia  kitabu cha risti  kimeandikwaje?
.
Naye Joshua Antoni alisema Kateksta huyu amekuwa   ombaomba kwa fedha za aina mbalimbali kwetu hata mihuri na risti zitolewazo kwenye kitabu cha risti tofauti na mlengo wa kanisani batili hatutambui zinafanya shughuli  ipi? Na zipo kwenye  kitengo  gani? Pia hazina Baraka kwa Mapadri wote,Baba  Paroko  na Askofu  Rodriki Minje.

2008-2009 kanisa katoriki jimboni hapo lilipata kashfa ya Kateksta  selestan   Amubi  kufumaniwa na mwanamke  wa Kinyarwanda Ngirwa Kamkara‘21’wakiwa  hana  nguo  saa 5:45 jioni  katika kata ya Majengo guest ya  Mayunga B ambapo  mwanamke huyo  alikimbia na nguo za Katekista  huyo.

Mwenyekiti wa  umoja wa wapiga  picha  wilaya  ya  kahama ‘’UWAPIKA’’Charles  Richard shinwa akizungumza na waandishi wa habari jimboni hapo  alisema  tumekuwa  tunabaguliwa  na  kutozwa shs,5000  kwa  kila  mpiga picha za  kawaida mmoja,mchukua video shs,10,000-12,000  na  baisikeli shs.700,pikipiki shs.1500 toka 2013-2014.

Bw,Shinwa  alisisitiza  jambo  hili la Katekista  kufanya  Ubaguzi  kwa  baadhi ya wapiga picha waingipo na kutozwa na wapo wasiotozwa  kuna waaumini  ambao  wanasari hapahapa mpaka sasa nao  wanatozwa kiwango cha shs.4000 wengine hawatozwi hicho ndicho kilicholeta mtafaruku  kati  ya  Katekista Samson Magoke na wadada wawili wanaoshirikiana naye wametuletea vitambulisho batili na risti zenye mhuri  Usiotambulika.

‘’Tumewekewa mistari miwili ya waaumini kupita ili wapigwe picha inatuchanganya wakati wa kupiga picha maana mhusika anakuwa  upande  mwingine  na sisi wapiga picha tupo upande mwingine huku tumelipishwa fedha na kuwekewa  masharti ya kupewa kitambulisho  mwisho wa shughuli tunawarudishia kitambulisho ambacho  hakina mhuri unaotambulisha ipasavyo’’.alisema Bw,Shinwa.

 Waandishi wa habari walivyomtafuta Katekista Samson Magoke ili atoe ufafanuzi wa tozo za wapiga picha na waumini wanaopiga picha alisema fedha zinazotozwa ni kusaidia wanaofanya usafi wa ndani na nje ya kanisa  hili  licha ya kutotangaza ila ni utaratibu wa kwetu sisi viongozi tulioweka  kuanzia 2012-13  hatukuwashirikisha Mapadri,Baba Paroko na  Askofu  Rodrck  Minje.

Baba paroko jimbo la katoriki  kahama  Robert Lujura alisema sina taarifa ya aina hiyo nitafanya kikao na katibu wa jimbo,Katekista huyo kwa maelezo  ya ufasaha kwa jambo hili  lenye Uchuuzi wa waaumini na wapiga picha waingiao  kanisani bila kuwatangaziwa waumini  na wapiga picha  kama kutakuwa na utaratibu wa kuwatoza fedha za kuingia kanisani  ikiwa na  baiskeli  na   pikipiki.

‘’Hili  jambo  ni  la ajabu na  aibu  kwa  Katekista kujifanyia maamuzi yenye  muono  wa  kibinafsi  pasipo  kufuata  neno la mungu  na  utaratibu wa kanisa  katoliki ulivyo na unavyofanya kwa nyakati hizi za ufufuo wa yesu  kwa  kiongozi wa kanisa kafanya makosa makubwa kwa makusudi  ya  uroho  wa tamaaya  fedha’’alisema Baba Paroko.

Upande wa Askofu Rodrick Minje alivyotafutwa na waandishi wa habari kwa njia ya  simu  haikupatikana ili kupata ufafanuzi wa michango inayotozwa  kanisani  kwa utaratibu  wa Katekista Samsoni Magoke aliokuwa nao  tangu 2012-13 mpaka  sasa anaendelea  kuwatoza waumini  na  wasiokuwa  waumini  kwa kiwango kikubwa.
                                                       MWISHO

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni